Sababu zinazopelekea Mwanamke Kupata Hedhi Mara Mbili au Zaidi Ndani ya Mwezi Mmoja
Mzunguko wa kawaida kwa wanawake ni siku 28
na Hedhi huenda siku 3-7 lakini wapo ambao mzunguko unakuwa siku 21 hadi 35 kutokana na sababu mbali mbali,
Kupata Hedhi mara mbili hujulikana pale ambapo
mwanamke katika mwezi au mzunguko wa siku 28 akatokwa na Damu ya Hedhi mara mbili
mfano anakaa siku 14 anapata Hedhi huyu anahesabika amepata Hedhi mara 2 ndani ya mwezi mmoja.
Mambo Yanayosababisha kupata Hali ya Namna Hii.
>>> Matumizi ya madawa ya Uzazi wa mpango,
Dawa hizi zina vichocheo homoni viwili kwa
Hivyo homoni zinaweza kuchochewa kuzidi na kupelekea Hedhi mara 2
>>>Uvimbe kwenye kizazi, Unafanya kizazi kishindwe kukaza na kushindwa kuzuia Damu kutoka
>>> Ugonjwa wa Polycystic ovaries syndrome,
Huu Ni Ugonjwa unaotokana na mwanamke kuwa na homoni ya kiume
Yaani "Androgen" kiasi kikubwa na hupelekea vifuko vidogo katika Mayai
>>> Ugonjwa wa Endometriosis ambao tishu kwenye mji wa Mimba zinaota kwenda nje
>>> Msongo wa mawazo husababisha mabadiliko ya kikemikali katika mwili
>>>Kutoa Mimba, hudhoofika Mayai na kufanya homoni zibadilike
>>> Ugonjwa wa PID maambukizi ya bacteria katika mji wa Mimba hupelekea Damu nyingi kutoka
>>> Kuwa na uzito mkubwa sana au mdogo hupelekea mabadiliko katika mwili
>>>Kuwa na ujauzito hasa mtoto akitungwa nje ya mji wa Mimba
>>>Kukoma Hedhi kipindi ambacho homoni ya estrogen inashuka kiwango
>>>Kuwa na Magonjwa ya Zinaa, kisonono Kaswende klamidia
>>>Kansa ya kizazi, Tezi ya Thyroid kutofanya kazi vizuri
>>> Mabadiliko ya Hali ya hewa au mazingira, Mazoezi makali au kupita kiasi
Kama Una Changamoto Yoyote Ya Kiafya Unaweza Kupata Msaada Kutoka Kwetu Kwa Namna.
1. Tukuhudumie Ukiwa Hukohuko Ulipo, Hapa Utatakiwa Kutupigia Simu 0684362870
2. Ufike Ofisini Kwetu Kwaajili Ya Vipimo, Ushauri na Tiba.

0 coment�rios: