*Kwanini Dawa Nyingi Unazotumia Hazikusaidii Kupata Ujauzito?*
Wanawake wengi sana wanafanya kosa hili hapa pindi wanapotaka kubeba mimba. Kosa lenyewe ni kuwa,
Wanapomwona mwanamke mwenzao ambaye alihangaika kupata ujauzito na baadae wanamwona amepata ujauzito.
Wanaanza kwa kuuliza ni dawa gani iliyomsidia mwanamke huyo kupata ujauzito?
Matokeo yake ni kwamba, jibu watakalopata ndio wanaanza sasa kuitafuta dawa hiyo ili na wao waitumie.
Wanafanya hivyo bila kujua, mwenzao alikuwa anasumbulia na nini na ile dawa ilienda kutibu nini hadi mwenzao kapata ujauzito.
Mwisho wa siku wanajikuta kuwa wameshaipata hiyo dawa na wanaanza kutumia.
Watatumia hadi itakapoisha, na baadae wanashangaa siku, wiki, miezi, miaka inapita.
Wao hawapati ujauzito, wakati mwenzao alitumia dawa hiyo hiyo kabla hata hajamaliza dozi alipata ujauzito.
Happ ndipo unaanza kujiuliza tatizo liko wapi, mbona haujapata ujauzito kama mwenzako?
Jambo usilolijua ni kuwa, dawa haina shida nasema hivi kwasababu kila dawa unayoiona.
Imetengezwa kwa ajili ya kutatua tatizo fulani. Kwahiyo ikiwa dawa hiyo ilitengenezwa kwa ajili ya kumaliza hilo tatizo.
Basi muhusika (au mtumiaji) wa hiyo dawa akitumia itamsaidia kumaliza tatizo alilokuwa nalo na atapata mtoto.
Wakati huo huo kwa mwingine akitumia dawa hiyo hiyo, haiwezi kumsaidia na kupata mtoto.
Kwasababu tatizo ulilo nalo wewe sio sawa na tatizo alilo nalo mwenzako.
Kwahiyo, kabla ya kutumia dawa yoyote ile hakikisha ya kwamba unajua tatizo ulilo kuwa nalo na unajua kuwa hiyo dawa inaenda kutatua tatizo hilo ulilo nalo
Vinginevyo zaidi ya hapo, utatumia dawa ya kila aina, dawa za kila kampuni, utatumia dawa za hospitali na za kienyeji.
Utapoteza pesa nyingi, lakin ikiwa dawa utakayotumia haiendani na tatizo ulilo kuwa nalo huwezi kupata ujauzito.
Utabaki kushuhudia tu kwa wenzako, halafu kwako unashangaa kwanini dawa inadunda?
Jibu ni rahisi tu, TATIZO lako na kazi inayoenda kufanya DAWA utakayotumia ni vitu viwili tofauti. Ndio maana tatizo lako haliishi.
Suluhisho lake ni nini sasa?
Suluhisho pekee ni wewe kujua chanzo cha tatizo lako (au kutobeba mimba) ni nini?
Ukishajua tafuta mtaalamu atakaekusaidia kukupatia tiba itakayoenda kumaliza hilo tatizo lako.
Ukifanya hivi utapata ujauzito. Vinginevyo ni shuhuri pevu.
Labda nikuuibie tu siri.
Matatizo mengi ambayo yanawakumba wanawake na yanayosababisha wasibebe mimba, tatizo kubwa ni moja tu, ambalo ni...
... HORMONAL IMBALANCE (kuvurugika kwa homoni)
Hayo matatizo mengine unayoyaona wewe, matatizo kama vile...
Uvimbe kwenye kizazi au mfuko wa mayai, kutoona siku zako, hedhi isiyo na mpangilio, kutokwa na mabonge (au kama vipande vya nyama) wakati wa hedhi.
Kupata maumivu makali wakati unakaribia hedhi au wakati wa hedhi yenyewe, matiti kuuma (au kujaa), kukosa ute wa uzazi,
Kukosa hamu ya tendo la ndoa, kutofurahia tendo, ukavu ukeni, kutokwa na hedhi nyeusi sana, n.k
Matatizo yote hayo huwa yanasababishwa na HOMON IMBALANCE.
Tatizo ni kwamba wengi wanapotaka kutatua changamoto hizo.
Huwa wanadili na tatizo kama lilivyo na sio kiini cha tatizo ambacho ni kuvurugika kwa homoni.
Kwa mfano, mtu ana uvimbe kwenye kizazi baada ya kutibu kiini cha tatizo huwa anataka kuondoa tatizo lilioko ambalo ni kuondoa UVIMBE.
Uvimbe huu atauondoa kwa njia mbalimbali mfano kufanyiwa upasuaji au kuchukua dawa itakayoondoa uvimbe huo.
Na huku anasahau kuweka homoni zake sawa.
Na hapo ndipo anapokuja kushangaa, uvimbe umeisha lakini mimba habebi. Kwanini?...
Kwasababu, kiini cha tatizo hakijaondolewa ambacho ni homoni kutokuwa sawa.
Na hata kwenye upande wa homoni, hii ni mada pana sana. Kwani...
Kuvurugika kwa homoni maana yake ni kwamba aidha homoni zinazidi kuliko kawaida au zinapungua kuliko kawaida.
Huenda ikawa wanawake wawili wote wana tatizo la homoni kutokuwa sawa.
Lakini, matibabu yake huwa tofauti na mwingine. Kwasababu ya dalili watakazoonyesha watu hawa.
Kiufupi ni kwamba, dawa zote unazotumia kuweka homoni sawa ni za muda mfupi.
Yaani zinafanya kazi ndani ya muda mfupi tu. Baada ya muda huo kupita hali inarudi pale pale.
Hii yote ni kwasababu ya mtindo wa maisha tunayoishi, madawa tunayotumia, vyakula tunavyokula (vingi vina kemikali na vimetoka viwandani)
Mafuta tunayotumia (ya kupaka au ya kupikia), vipodozi unavyotumia, n.k.
Kwahiyo, njia pekee itakayoweza kukusaidia ni wewe kutumia dawa hizo ambazo zitakusaidia kuweka homoni zako sawa.
Lakini pia, upate muongozo mzuri utakokusaidia ku mantain hizo homoni zako zisivurugike tena.
Nina mengi ya kukuambia, lakini acha tu tuishie hapa.
Haya yote niliyokuambia ni matokeo niliyoyapata baada ya kuongea na baadhi ya wanawake wenye Changamoto za KUTOSHIKA MIMBA ndo nimekuja kugundua hayo.
Kwahiyo wewe kuwa makini hata pale utakapo nunua dawa basi jitahidi ufahamu na namna itakayokuwezesha ku maintain homoni zako zisicheze tena baada ya kumaliza kutumia dawa.
Nakutakia mafanikio mema!
Mimi ndugu yako.
Mzamilu Baraka